Tuesday, May 3, 2016

POKEA BARAKA ZAKO KWA JINA LA YESU KRISTO

BWANA YESU ASIFIWE

Bwana,akujibu siku ya dhiki.


Jina la Mungu wa Yakobo likuinue
Akupelekee msaada toka patakatifu pake
Na kukutegemeza toka sayuni
Azikumbuke sadaka zako zote
Na kuzitakabali dhabihu zako
Akujalie kadiri ya haja ya moyo wako

Na kuyatimiza mashauri yako yote

Na tuushangilie wokovu wako kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu
Bwana akutimizie matakwa yako yote
Sasa najua Bwana amuokoa masihi wake
Atamjibu toka mbungu zake takatifu


Kwa matendo makuu ya wokovu ya mkono wake wa kuume.

Hawa wanataja magari na hawa farasi bali sisi tutalitaja jina la Bwana Mungu wetu
Wao wameinama na kuanguka
Bali sisi tumeinuka na kusimama

Bwana umuokoe mfalme
Utuitikie siku tuitayo

AMEEN

Sunday, May 1, 2016

TUMTAFUTE MUNGU MAADAMU ANAPATIKANA.

kanisa Zanzibar


BWANA YESU atukuzwe ndugu.
Karibu tujifunze.
Mithali 8:17 ''Nawapenda Wale Wanipendao, Na Wale Wanaonitafuta Kwa Bidii Wataniona.''.
-Maombi ni njia ya mawasiliano kati ya MUNGU na watoto wake waliosafishwa kwa damu ya mwanawe wa pekee YESU KRISTO. -Maombi ndio mawasiliano kati yetu wanadamu na MUNGU Baba yetu. Ili uhusiano wetu na MUNGU uwe hai lazima tuwe waombaji. Zaburi 62:8.'' Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; MUNGU ndiye kimbilio letu. ''
-MUNGU huongea na sisi kwa njia ya neno lake kupitia kusoma kwetu Biblia na huongea na sisi kupitia watumishi wake, na sisi tunaongea na MUNGU kwa njia ya maombi, hivyo ili uhusiano wetu na MUNGU uwepo lazima tuwe na muda wa maombi.
-BWANA Anatutaka Tumtafute Kwa Maombi
- Tumtafute Kwa Matoleo
-Tumtafute Kwa Matendo Mema
-Tumtafute MUNGU Kwa Kumtegemea Yeye Peke Yake.
-Tuombe Kwa Jina La YESU KRISTO Pekee(Yohana 14:13-14, Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili BABA atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya. )
-Kila mtu ana wajibu wa kumtafuta MUNGU kwa maombi
- Maombi ni maisha ya waenda mbinguni.
-Maombi ni mkono mrefu wa kupokea baraka kutoka kwa MUNGU.Maombolezo 3:25 "BWANA Ni Mwema Kwa Hao Wamngojeao, Kwa Hiyo Nafsi Imtafutayo.".
-Ndugu mtafute BWANA.
MAOMBI NI MAISHA YA WATEULE, NA ILI UFANYE VYEMA NI MUHIMU KUJUA HAYA.
1. Tumtafute MUNGU Hata Hivyo MUNGU Hawi Mbali Na Kila Mmoja(Matendo 17:26-27, Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili wamtafute MUNGU, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.).
2. Tumtafute MUNGU Kwa Imani(Waebrania 11:6, Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye MUNGU lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao. ).
3. Tuombe, Tumtafute Na Tubishe Kwenye Ufalme Wake ili tupokee baraka (Mathayo 7:7, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; ).
4. Mjue Kwanza MUNGU kwa kumcha na ukizingatia kumcha MUNGU hakika utakuwa unamjua. (Mithali 2:4-5, Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika; Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, Na kupata kumjua MUNGU.).
5. Omba bila kukoma na uzimzimishe ROHO MTAKATIFU.(1 Thesalonike 5:17-19 ,ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya MUNGU kwenu katika KRISTO YESU. Msimzimishe ROHO;)
MUNGU Ameahidi Kwamba Tutamuona Kama Tu Tukimtafuta Kwa Bidii(Yeremia 29:13, Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote. ).
Tumtafute BWANA Wa Mabwana Maadamu Anapatikana, Tumwite Maadamu Ya Karibu Ila Mtu Mbaya Aache Dhambi Na Arejee Kwa BWANA Naye Atamrehemu(Isaya 55:6-7, Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu; Mtu mbaya na aache njia yake, Na mtu asiye haki aache mawazo yake; Na amrudie BWANA, Naye atamrehemu; Na arejee kwa MUNGU wetu, Naye atamsamehe kabisa. ).
BWANA YESU Anatupenda Sana.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

UNAZIFANYIA NINI SIKU ZAKO ZA KUISHI DUNIANI?



BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Tuko leo duniani Kwa kusudi maalumu la MUNGU.
Tuko leo duniani Kwa sababu maalumu ya Muumbaji.
Tuko Leo duniani Kwa mpango maalumu Wa MUNGU.
Tuko Leo duniani Kwa kipindi maalumu.
Tuko Leo duniani Kwa muda maalumu.
Muda maalumu ukiisha kila mmoja ataondoka.
Mhubiri 3:1-2 ''Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa; ''
Kila jambo hakika lina wakati wake.
Muda wa kuishi mwanadamu ni mfupi sana ukilinganisha na milele ijayo.
Milele ijayo ina makazi ya aina mbili;
kuna makazi ya watakatifu yaitwayo uzima wa milele na kuna makazi ya watenda dhambi waliokataa kuokoka wangali wakiishi duniani, makazi yao hao yanaitwa jehanamu ya moto kwenye mateso ya milele.
Wakati huu mwanadamu anaishi duniani ndio wakati wa kuamua ni wapi atakuwa milele ijayo.
Siku za kuishi duniani za mwanadamu ni chache sana na hizo chake mwanadamu anatakiwa azitumie katika kumcha Muumba wake na kuishi maisha ya wokovu ulio pekee katika KRISTO YESU.
Miaka yako michache ya kuishi duniani unaitumiaje?
Ayubu 14:1-2 ''Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe.''
Biblia inathibitisha kwamba miaka ya mwanadamu kuishi duniani ni michache sana ukilinganisha na miaka isiyohesabika ya milele ijayo.
Katika miaka hii michache ya mwanadamu kuishi MUNGU kwa upendo wake mkuu akaamua kuleta Wokovu kwa wanadamu.
Wokovu ni mpango wa MUNGU kumuokoa mwanadamu. Na Mpango huo wa MUNGU kumuokoa mwanadamu uko pekee katika KRISTO YESU, BWANA na Mwokozi wa watu wote watakaomtii.
1 Yohana 4:14-15 ''Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa BABA amemtuma MWANA kuwa MWOKOZI WA ULIMWENGU. Kila akiriye ya kuwa YESU ni Mwana wa MUNGU, MUNGU hukaa ndani yake, naye ndani ya MUNGU.''
Mpango maalumu ni kila mmoja aokoke na aishi maisha matakatifu.
Anayeokoa ni BWANA YESU na yeye siku zote anawangoja wanaompokea na kulitii Neno lake ili awape uzima wa milele.

BWANA YESU analithibitisha hilo kwa kinywa chake akisema;
''Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu. Mimi na Baba tu umoja.-Yohana 10:28-30''
Kwa maandiko hayo ukweli ni kwamba hakuna mwanadamu hata mmoja anayedai yeye yuko upande wa MUNGU wakati anakataa kuokolewa na YESU KRISTO.
=Hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye atasema yeye ana MUNGU wakati huo huo yeye hataki kuokolewa na YESU KRISTO.
=Ukweli ni kwamba kila mwanadamu anayeutaka uzima wa milele ni lazima awe chini ya YESU KRISTO.
=YESU KRISTO na MUNGU BABA ni umoja tena ni mmoja, mipango yao ni mimoja kama andiko hapo juu linavyosema.
Na kwa Biblia ya kingeleza andiko hilo la Yohana 10:30 imeandikwa hivi '' I and my Father are one.''
=Hivyo hakuna mwanadamu aliye upande wa YESU KRISTO harafu tena eti huyo mwanadamu asiwe upande wa MUNGU.
=Hakuna mwanadamu aliye upande wa MUNGU kama mwanadamu huyo hayuko upande wa YESU KRISTO.
Mwanadamu asiye upande wa YESU KRISTO huyo mwanadamu anakuwa pia hayuko upande wa MUNGU na kama hayuko upande wa MUNGU moja kwa moja mwanadamu huyo anakuwa hahusiki na uzima wa milele.
Yohana 3:16-18 ''Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana MUNGU hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa MUNGU.''
Ni Muhimu sana kumuamini YESU KRISTO, kumpokea na kuliishi neno lake.
Najua kuna maelfu ya watu wameshampokea BWANA YESU na wanaishi maisha matakatifu, na najua pia kuwa kuna watu bado hawajaokoka lakini kupitia ujumbe huu ambao ROHO wa MUNGU amenipa basi wataokoka, maana miaka inaenda na muda wa kuishi mwanadamu ni mchache sana ukilinganisha na milele ijayo.
Ndugu zangu,Kwa jinsi kila tunavyoiona siku mpya ndivyo pia muda maalumu Wa kukaa duniani unaendelea kuisha.
Kabla muda wa kukaa duniani haujaisha ni muhimu sana kila mwanadamu kuokoka na kuanza kuishi maisha matakatifu.
Kabla ya muda wa kuishi duniani haujaishi Ni muhimu sana kumwabudu MUNGU katika Roho na kweli.
Kanisani Hatuhitaji Uzoefu Bali Utakatifu.
Uzoefu Wetu Wa Ibada Na Miaka Yetu Mingi Ya Kuwa Washirika Wa Kanisa Havina Maana Hata Moja Kama Hatuishi Maisha Matakatifu.
Ndugu yangu, ishi maisha matakatifu maana hilo ndilo kusudi la MUNGU kwa mtu baada ya mtu huyo kumpokea YESU KRISTO kama BWANA na Mwokozi wake.
Tunayo neema ya MUNGU BABA maana Hatuishi duniani Kwa bahati mbaya Bali tunaishi Kwa sababu ni haki yetu kuishi aliyotupa JEHOVAH MUNGU muumba wetu.
Katika hiyo haki yetu ya kuwa hai sasa, MUNGU anataka tuitumie hiyo haki yetu katika utakatifu na kumtumikia.
shetani naye kwa sababu anaujua uzuri wa mbinguni kwa sababu aliwahi kuishi huko kabla ya kufukuzwa, basi huyo hujaribu kuwafanya wanadamu wasiende huko uzima wa milele.
shetani amepanda vitu vingi kwa siri ili tu kuwafanya wanadamu wamuasi Muumba wao.
shetani ameleta dini nyingi ili tu kuwavuruga wanadamu ili wasiokoke.
Hata walimu wengi wa uongo shetani amewaleta ili tu kuwafanya wanadamu wasimpokee YESU hata wakaokoka.
Kuna siri zingine shetani hataki watu wengi wajue ndio maana analeta vita kubwa mno ili watu wasifundishwe kweli ya MUNGU. Lakini habari njema ni kwamba jina YESU KRISTO ni ngome imara, tukikimbilia tunakaa salama.
Mithali 18:10 ''Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.''
Katika JEHOVAH linapatikana jina la YESU KRISTO.
Katika jina la YESU KRISTO kunapatikana ushindi na mamlaka kuu ya kuangamiza hila zote za shetani.
Waliompokea YESU KRISTO hao wamefanya agano na MUNGU BABA.
Agano hilo ni mapatano matakatifu ambayo mwanadamu anatakiwa ayazingatie ili baada ya muda wake wa kuishi duniani kuisha aende uzimani.
Masharti Mawili Ya Agano Kati Mwanadamu Na MUNGU Ni
(1)Kutii Sauti Ya MUNGU
(2)Kushika Agano La MUNGU.
=Kutii sauti ya MUNGU ni kumpokea YESU KRISTOna kuanza kuishi maisha matakatifu.
=Kushika agano la MUNGU ni kuifuata Biblia kile inachofundisha na kukiishi, pia kushika agano la MUNGU ni kuyazingatia maungano ya ukiri wako wa kumpokea YESU. Yaani sala ya toba ile uliyoongozwa ni ungamo ambalo unatakiwa ulishike siku zote.
Ndugu yangu naomba pia ujue kwamba Kusudi La MUNGU Huonekana Mwishoni Na Sio Mwanzoni.
Asichokizungumza MUNGU Huwa Hakitendi.
Na Alichokizungumza MUNGU kwamba atakitenda hakika hutenda.
Tunamwita MUNGU Ni Mwaminifu Kwa Sababu Alilosema Hulitimiza.
MUNGU alisema watakaompokea YESU KRISTO na kuishi maisha matakatifu wataurithi uzima wa milele. Hicho MUNGU alikisema na atakitimiza.
Ukiokoka ni muhimu pia kumtimikia MUNGU.
Mtumikie MUNGU kwa kila kitu chako iwe ni sauti yako au mali yako.
MUNGU Anafanya Kazi Na Wanaompenda, Sio Waliookoka Bali Waliookoka Na Wanampenda.
Waliookoka na kumpenda MUNGU hao MUNGU hufanya kazi nao, huwatumia katika matendo makuu na baraka kuu.
Warumi 8:28 '' Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote MUNGU hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. ''
Ndugu Mpendwa, jambo jingine muhimu kujua ni kwamba Kuna Vitu Hutakiwi Kufanya Haraka Kama Tu Vitu Hivyo Una-share Na MUNGU.
Maana MUNGU Ana taratibu Zake Za Kukufanikisha Wewe Katika Baraka Hizo Njema.
Mfano;
Kama Umeomba MUNGU Akufanikishe Kupata Mchumba Sahihi Kwanini Uwe Na Haraka Kana Kwamba Jambo Hilo Unaliamua Wewe Peke Yako?
Ndugu, Kama Umemshirikisha MUNGU Basi Husika Na MUNGU Zaidi Kabla Ya Mengine.
Husika Na MUNGU Kwa Maombi.
BWANA YESU anasema;
'' Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili BABA atukuzwe ndani ya MWANA. -Yohana 14:13''
Jambo jingine nataka ufahamu ni kwamba Kuna Neno la MUNGU na kuna neno la shetani.
Neno la MUNGU ni Uzima tena ni uhai lakini wanadamu wengi hupenda zaidi neno la shetani kuliko Neno la MUNGU.
ni wakati wa kujitafakari sana kila Mtu.

je unalitendea kazi Neno la nani?
Neno la MUNGU ni Biblia na hilo Neno la MUNGU ndilo unalotakiwa kulitendea kazi.
Neno la shetani ni kila kitu kinachopingana na Biblia kiwe ni kitabu au ni maneno ya watu wanayoyatamka kwako.
2 Yohana 1:9-11 ''Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya KRISTO, yeye hana MUNGU. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana BABA na MWANA pia. Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu. ''
Jambo la jingine nataka ufahamu ni kwamba Kuna KRISTO na kuna mpingakristo.
KRISTO kazi yake ni kupeleka wanadamu Uzima wa milele.
mpingakristo kazi yake ni kupeleka wanadamu jehanamu.

2 Yohana 1:7-8 '' Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea duniani, wasiokiri ya kuwa YESU KRISTO yuaja katika mwili. Huyo ndiye yule mdanganyifu na mpinga Kristo. Jiangalieni nafsi zenu msiyapoteze mliyoyatenda, bali mpokee thawabu timilifu.''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichaka chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.

AU HAMJUI?



BWANA YESU atukuzwe.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Neno la MUNGU la leo linamtaka kila mwanadamu kujua, kuchukua hatua na kubadilika katika mfumo wake wa maisha.
Au hamjui?
''Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa MUNGU? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi-1 Kor 6:9-10''
Katika ambao hawataurithi ufalme wa MUNGU ni pamoja na Waasherati, waabudu sanamu, wazinzi, wafiraji, walawiti, wezi, watamanio, walevi, watukanaji na wanyang'anyi.
Watenda dhambi wote hawataurithi uzima wa milele kama hawatatubu kipindi hiki wakiwa hai duniani.
Anayesamehe dhambi ni BWANA YESU pekee hivyo kama kuna mtu pia hamwitaji YESU basi huyo ndugu hauhitaji uzima wa milele.
Biblia inataka kila mwanadamu ajue hivyo ili aamue kama anautaka uzima wa milele au hautaki.
Kuna watu inawezekana kabisa wao sio waasherati lakini ni waabudu sanamu, hao wasipotubu wakati huu wakiwa hai hawawezi kuurithi ufalme wa MUNGU.
Kuna watu sio waabudu sanamu lakini ni wazinzi, hao hawataurithi ufalme wa MUNGU wasipotubu wakati huu wakiwa hai.
Kuna watu inawezekana kabisa sio wazinzi wala hawajawahi kutoka katika ndoa zao lakini tatizo lao hufanya mapenzi kinyume na maumbile, Biblia inawaita wafiraji, hao nao wasipotubu sasa wakiwa hai hakika uzima wa milele hauwahusu.
Ndugu mmoja anasema ''mradi sitoki nje ya ndoa'' lakini huyo huyo hufanya mapenzi kinyume na maumbile na kujivunia kilo nyingi za dhambi kila siku maana uovu huo ni mbaya sana na una madhara mengi sana kiroho na kimwili.
Kwa sababu Biblia kwa ukali kabisa imelitumia hilo neno ''wafiraji''
basi ngoja na mimi nilitumie ili kusema ukweli huu kwamba hakuna mbingu ya watu waliokuwa wafiraji.
Wewe mume unayemfira mke wako, huo ni uovu mkuu, tubu na acha uovu huo maana unapotenda hayo naomba utambue pia kwamba usipotubu kuna jehanamu inawangoja wafiraji wote. ukitubu leo na kuacha dhambi hakika unasamehewa.
Mathayo 3:2 ''Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. ''
Wewe mke unayekubali kufirwa, huo ni uovu mkuu na kama usipoacha kuingiliwa huko kinyume na maumbie kuna ziwa la moto linalowangoja wafirwaji. tubu na acha uovu huo, kama unadhani huo ni upendo basi huo ni upendo wa kishetani, ni kamba ya kukuvuta taratibu hadi jehanamu. tubu na geuka leo maana watenda dhambi hawana nafasi katika ufalme wa MUNGU. Lakini ukitubu leo na kuokoka na kuacha uovu huo utapona.
ufiraji kama ulivyo ulawiti ni uovu mkuu na Biblia iko wazi ikisema kwamba watendao uovu huo hawataenda uzima wa milele. Dawa ni kutubu, kuacha uovu huo na kuanza kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
kuna watu huwalawiti hata watoto wao wa kiume na wa kike.
Kuna vijana hulawitiwa.
Kuna watu huwalawiti hadi watoto wadogo.
Kuna watu hulawiti hadi wanyama.
Huo ni uovu mkuu na Biblia iko wazi sana ikisema;
''katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa MUNGU.-Wagalatia 5:21''
Inawezekana kabisa kuna watu sio wazinzi lakini wao ni walevu, huiona dhambi ya ulevi ni ndogo lakini Biblia iko wazi sana hapo juu kwenye andiko la kwanza ikisema walevi hawataurithi ufalme wa MUNGU.
''Kunywa kidogo ila usilewe'' ni ajenda ya shetani iliyowekewa muhuri na baadhi ya viongozi wa kanisa wasioipenda mbingu.
Je hamjui?
2 Kor 6:14 ''Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? ''
Nuru ni wokovu na kuishi katika utakatifu kama Biblia inavyoelekeza.
Giza ni shetani na mambo yake yote.
Watu wa MUNGU wanaotarajia uzima wa milele hawatakiwi kujichanganya na mambo ya giza katika maisha yao.
kuna watu kwa waganga wanaenda na kanisani wanaenda, huo ni upagani hata kama kanisani uko kila wiki.
acha mambo ya giza na dumu katika kanisa ukidumu pia katika kulitii Neno la MUNGU.
Siku hizi kuna mashoga hadi kanisani. ni machukizo na Biblia iko wazi sana ikisema kwamba hakuna mbingu ya washoga. ndoa za mashoga ni ndoa zenye agano la shetani, ni ndoa ambazo machozi ya furaha hayatoki wakati wa kufunga ndoa lakini machozi ya huzuni yanaweza kutoka kwa kila mtenda dhambi hiyo kama ndoa hiyo itadumu hadi kifo maana baada ya kifo cha mwenye dhambi kuna ziwa la moto baadae.
Biblia iko wazi kabisa kukataza ushoga.
Kuna matukio mawili yaliwahi kunishangaza sana baada ya kuyasikia. tukioa la kwanza kuna kwaya moja, mmoja wa waimbaji mahiri sana wa kiume kwenye kwaya hiyo ni shoga. sikuamini lakini mmoja wa waimbaji wa kwaya hiyo ndiye aliyeniambia huku akidai yeye mwenyewe aliwahi kutakwa na yule shoga, akakataa na kumkemea na kumripoti kwa mchungaji wa kanisa. baadae ilikuja kuwa wazi juu ya mwimbaji huyo mwenye kipaji na tegemeo katika kwaya hiyo. ni hatari sana. hilo ni giza katikani ya nuru.
Hakutakiwi kuwapo mtu wa hivyo katika kundi la wateule wa MUNGU. Ni machukizo makuu hayo na Biblia iko wazi ikisema hakuna uzima wa milele kwa mashoga yaani kwa wanaume wanaofirwa na wanaofira.
Siku moja pia kuna mtumishi mmoja alishuhudia mbele ya kanisa mahali fulani juu ya tabia ya mume wake kumwingilia kinyume na maumbile kila siku. kwa jinsi ndugu yule alivyokuwa amesimama kiroho nilitamani kulia.
Ni hatari sana kuolewa na mtu asiye na hofu ya MUNGU.
Ni hatari sana kuoa mwanamke mpagani.
Ukiwa na mwenzi wa ndoa mwenye tabia hiyo ni heri kuachana naye kabisa, maana heri upate uzima wa milele kuliko kupata jehanamu iliyozaliwa na ndoa.
Hakutakiwi kuwepo giza katika nuru.
1 Yohana 1:5-7 '' Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba MUNGU ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake.Tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli; bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake YESU, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. ''
Giza ni giza na nuru ni Nuru, ni heri kuikimbilia Nuru ambayo ni BWANA YESU.
Au hamjui?
2 Kor 6:16 ''Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la MUNGU na sanamu? ''
Sanamu leo zinaabudiwa kwenye baadhi ya nyumba za ibada..
Sanamu leo imegeuka Mungu kwa baadhi ya watu.
Biblia iko wazi sana ikisema kwamba hakuna mapatano kati ya sanamu na kanisa la MUNGU.
Kwenda kwa waganga wa kienyeji ni kuabudu sanamu.
Kumwabudu Mariamu ni kuabudu sanamu.
Biblia iko wazi ikisema
''Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa MUNGU, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu. -Matendo 17:29 ''
MUNGU hayuko katika sanamu yeyote bali MUNGU yuko mbinguni.
BWANA YESU hayuko katika sanamu ya aina yeyote bali BWANA YESU yuko mbinguni.
Watakatifu wa zamani hawako katika sanamu yeyote bali wako mji mtakatifu wakifurahi kwa BWANA YESU.
Mwanadamu kujiita Mungu ni kujitengeneza mwenyewe awe sanamu na aabudiwe.
Ni uovu mkuu sana.
Biblia iko wazi sana ikisema
Zaburi 29:2 ''Mpeni BWANA utukufu wa jina lake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu.''
Kuna watu badala ya kumpa MUNGU heshima wao huzipa heshima sanamu zilizotengenezwa na wanadamu.
Tangu miaka yote katika Biblia MUNGU aliwaambiwa watu wake wavunje sanamu zote zinazoabudiwa na kunyenyekewa na wanadamu.
Tangu zamani MUNGU amekataza watu wake wasihesimu sanamu.
Kumb 7:5 ''Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga. ''
Je hamjui?
1 Kor 6:15 ''Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya KRISTO? Basi nivitwae viungo vya KRISTO na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!''
Tena, Je Hamjui?
1 Kor 6:16 '' Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? ''
Je Hamjui?
1 Kor 6:19 ''Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la ROHO MTAKATIFU aliye ndani yenu, mliyepewa na MUNGU? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;''
Mkristo aliyeokolewa na BWANA YESU huyo ni hekalu ya ROHO MTAKATIFU.
Huyo ni makazi ya ROHO wa MUNGU.
Kama mkristo huyo akianza dhambi ROHO wa MUNGU huondoka ndani yake, ni hatari sana ROHO wa MUNGU kuondoka katika maisha ya Mkristo.
Kanisa ni mwili wa KRISTO na kanisa na wakristo wote wanaomtii KRISTO YESU.
Kuna watu wameungwa na kahaba.
Hawa ni wale watenda dhambi, hao wameungwa na dhambi yaani wao na dhambi ni mwili mmoja hadi watakapotubu ndipo watatengwa na dhambi hizo.
Kama wewe unajiita Mkristo kisha humtii KRISTO hakika wewe hauna sehemu katika ufalme wake KRISTO. Tubu na rejea ili usamehewe.
Matendo 3:19 ''Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA; ''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichaka chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili

SIKU YA MWISHO SIRI HAZITAKUWA SIRI TENA.



BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Siku ya mwisho mambo yote yatakuwa peupe.
Isaya 13:9-11 '' Tazama, siku ya BWANA inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake. Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze. Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;''
Kazi moja kubwa itakayofanyika siku ya mwisho ni hukumu.
Hukumu hiyo itafanywa na BWANA YESU na siku hiyo kutakuwa na makundi mawili tu ya wanadamu; Kundi la kwanza ni watu wanaoenda uzima wa milele na kundi la pili ni watu wanaoenda jehanamu.
Siku hiyo hakutakuwa na siri tena.
Waabuduo halisi watajulikana siku hiyo.
Wanao igiza utakatifu wataonekana siku hiyo.
Wanaotumainia dini siku hiyo itajaulikana wazi.
Mambo ya siri yaliyofanywa na kila mwanadamu yote yatakuwa peupe.
Walioishi maisha safi ya wokovu wa BWANA YESU wataenda uzima wa milele.
Waliomkataa BWANA YESU siku hiyo wataenda jehanamu hata kama walitenda baadhi ya matendo mema, ila kumkataa tu BWANA YESU hapo watakuwa wameukataa uzima wa milele.
2 Petro 3:10-12 '' Lakini siku ya BWANA itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, mkitazamia hata ije siku ile ya MUNGU, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? ''

Ni siku ya furaha kwa waliookoka kisha kuishi maisha matakatifu na ni siku ya kujuta na kulia kwa walioukataa wokovu wa BWANA YESU.
Kila kitu kitakuwa wazi kabisa.
Mwanamke aliyekuwa anaisaliti ndoa yake kwa usiri mkubwa siku hiyo itajulikana hadharani kwamba yeye ulikuwa msaliti.
Wewe baba ambaye una nyumba ndogo siku hiyo itajulikana wazi dhambi yako hiyo.
Wewe mfanyakazi wa serikali unayeiba pesa siku hiyo wizi wako utajulikana.
Wewe mchawi unayeroga watu kwa siri huku ukienda kanisani kama kujificha uovu wako huo watu wasijue siku hiyo dhambi yako hiyo itajulikana.
Wewe unayetapeli watu siku hiyo mambo yako yote yatakuwa peupe.
Wewe changudoa siku ya mwisho mambo yako yote yatakuwa peupe.
Biblia inaonya sasa ili mwenye sikio la kusikia aache dhambi na kutubu na kuokoka.
1 Petro 3:10-11 ''Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana. ''
Ndugu, je umelielewa andiko hilo?
Ni maonyo na maagizo muhimu kutoka kwa MUNGU aliye hai, akikuonya kwamba uache mabaya na utende mema.

Wewe ambaye huwa unafanya uovu kwa kumuogopa tu mchungaji, mchungaji akiwa karibu wewe ni mwema sana lakini mchungjai akiwa mbali unafanya dhambi, ndugu siku hiyo mambo yake yote yatakuwa peupe.
Wewe uliye na utajiri wa kishetani siku hiyo ya mwisho itajulikana.
Wewe unayetembea na hirizi siku hiyo mambo yako yote yatakuwa peupe na dhambi yako hiyo itakuwa dhahili.
Hakuna mwanadamu ambaye atasema ameonewa maana hukumu ya MUNGU iko wazi sana maana hata matendo yako mabaya yatazungumza.
Biblia inasema hivi kuhusu hiyo siku ya hukumu.
Ufunuo 20-12 ''Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.''
Ni siku ya kutisha, ni siku ambayo wanaojivunia kazi zao na utajiri wao havitawasaidia.
Kuna watu leo kila wakiambiwa waende kanisani wanasema wako busy kazini, lakini siku hiyo hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye atalipwa kulingana na kazi yake serikalini, bali atalipwa sawasawa na matendo yake.
Ni siku ya mambo yote Peupe.
Lakini pia iko furaha kubwa kwa watakatifu wa MUNGU waliosafishwa kwa damu ya YESU KRISTO.
Hatutakiwi tuishi kwa sababu tu tunaishi bali tunatakiwa tuishe kwa sababu KRISTO YESU anaishi ndani yetu.
Tuishi maisha matakatifu siku zote.
BWANA YESU anasema;
'' Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za BABA yangu, na mbele ya malaika zake.Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa.- Ufunuo 3:5-6 ''

Ndugu yangu, nakuomba futa utaratibu wako wa dhambi na anza kuishi maisha matakatifu ukiwa umeokoka.
Nakuomba katika maisha yako ufunge ukurasa wa dhambi kuanzia leo na fungulia ukurasa wa matendo mema kuanzia leo.
Sio lazima mawazo yako ya jana yawe ndio mawazo yako ya leo.
Kama jana uliwaza dhambi naomba leo uwaze kuokoka na utakatifu.
Okoka kisha ishi maisha matakatifu.
Kuendeleza mawazo ya jana yasiyokusaidia ni kujipoteza huku unajiona.
Matendo 3:19 ''Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA;''

✔Kumjua YESU KRISTO ni kuijua njia ya uzima wa milele.
✔Kumkataa YESU KRISTO ni kuukataa uzima wa milele
''Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni; ambaye sauti yake iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia.- Waebrania 12:25-26
Ndugu zangu ni muhimu sana kuanza kuishi maisha matakatifu.
Kama umeokoka hakika naomba utambue kwamba tumeokolewa na BWANA YESU ili tuishi maisha matakatifu.
Kama hujaokoka hakika nakuomba uokoke, kumbuka dunia na mambo yake yote yatapita.
Kama kuna dhambi unadhani huwezi kuicha nakuomba Kimbilia maombezi na uwe muwazi kujieleza mbele ya wachungaji, maana kufanya siri haitakusaidia bali kusema ukweli na kuhitaji maombezi utapona.
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichako chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili

KINYWA CHAKO KINAWEZA KUUMBA MAMBO YATAKAYOKUTESA BAADAE.



BWANA YESU atukuzwe.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Usikubali kuwa mwepesi kusema kwenye kila jambo maana mengine unayojinenea sasa yanaweza kuja kukutesa baadae.
Zaburi 34:13 ''Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.''
Kinywa chako kinaweza kuzalisha jambo baya au jambo jema kulingana na unavyojitamkia.
Mithali 18:21 ''Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.''
Mfano ulisema kwamba katika ukoo wenu mtu akimaliza tu La saba anaolewa au kuoa hivyo na wewe ukimaliza tu La saba utaoa/ kuolewa. Baadae umefika La saba ukafaulu na kiu ya kusoma ikaja. Unaweza ukasoma Kwa shida maana ulijinenea Kuwa ukimaliza tu La saba unaoa/ kuolewa.
Usikubali kujinenea mabaya maana mengine yanaweza kuja kukutesa baadae.
Hakikisha unajinenea mema sio mabaya.

Mithali 15:2 ''Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.''

Je, Kinywa chako kinatamka maarifa mazuri au kinatamka upumbavu?
Kama kinywa chako kinatamka maarifa mema hakika utavuna matunda yake mema.
Kama kinywa chako kinatamka upumbavu au mambo mabaya hakaika hayo yanaweza kuja kukutesa baadae kama hutaomba rehema na kuyafuta kwa damu ya YESU KRISTO.
Kinywa huwa kinaumba.
Kinywa kinaumba yale unayoyatamka.
Je unatamka nini kwa kinywa chako?
Hata wanaokulaani, hukulaani kwa kinywa hivyo kama unajinenea mabaya na wewe ndio hali itakuwa mbaya zaidi.
Kama kuna watu wanakutamkia mabaya hakikisha unafuta maneno yao kwa damu ya YESU na kwa jina la YESU KRISTO kupitia maombi.
Haribu kila mipango ya kinywa kinachokunenea mabaya,
Kataa kusudi hilo la giza.
Mithali 15:4 '' Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo. ''
Huwezi kusema kitu mdomoni kama kama kitu kicho hakiko moyoni mwako.
Ukimuona baba na ndevu zake anadanganya vibinti vidogo Kwa mdomo wake ujue moyo wake huyo baba umejaa uongo na machukizo, Tena moyoni wake jini mahaba ameweka kigoda na kukaa.
Na kabinti kanakodanganywa na kakakubali Kwa mdomo hako nako moyoni kumejaa dhambi na vitamaa vya kishetani.

Kama moyoni mwako umemjaza shetani hakika kinywa chako kitaonyesha ushetani.
Mithali 12:20 '' Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.''
Ukijaza moyoni utakatifu hakika kinywa chako kitathibitisha.
kile kilichomjaa mtu moyoni ndo kimtokacho mdomoni!!
Moyo ukijaa matusi, mdomoni utanena matusi tu kila wakati.
kuna baadhi ya watu hawawezi kuongea bila kutukana tusi lolote. Na walio wengi sasa hivi kutukana imekua kama fasheni.
Tumeambiwa kila neno baya tunalotamka mdomoni tutamtoa hesabu yake siku ya mwisho, kama hututafuta maneno hayo sasa kwa kutubu.
Warumi 3:12-14 ''Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja. Koo lao ni kaburi wazi, Kwa ndimi zao wametumia hila. Sumu ya fira i chini ya midomo yao. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.''
Maneno ya watu hutumika katika mambo mema.
Maneno ya watumishi wa MUNGU yana maana sana ila angalizo kwa watumishi ni hili;
Maneno ya mtumishi Wa MUNGU yanatakiwa yawe maneno ya kuwaponya watu na sio kuwaua.
Maneno ya kuwaponya watu wakati mwingine yanaweza kuwa Makali na ya makaripio makali sana na ya kuonya na kukemea Kwa ukali sana maana huko ndiko kuwaponya watu.
Mtumishi anayekutia moyo kwenye dhambi yako Huyo anakuua wala hakuponyi.
Mtumishi anayekukemea huyo anakuponya.

Kwa mtumishi wa KRISTO kunatakiwa litoke Neno la kuponya na sio kuua.
Najua kila aliyeokolewa na BWANA YESU huyo ni mtumishi Wa KRISTO hivyo ni muhimu sana wote tuwe na maneno ya kuponya na sio kuua.

Matendo 4:31 '' Hata walipokwisha kumwomba MUNGU, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa ROHO MTAKATIFU, wakanena neno la MUNGU kwa ujasiri. ''
MUNGU anauangalia utakatifu wako siku hadi siku.
Hivyo ni muhimu kuongeza utakatifu na sio kuupunguza utakatifu au kuufuta kabisa utakatifu.
Ukidumu katika utakatifu hiyo ni Kwa faida yako peke yako na sio mtu mwingine yoyote.
Kinywa ni muhimu sana katika kukamilisha utakatifu wako.
Kuna watu wameokoka miili ila vinywa vyao havijaokoka kabisa maana hutamka matusi kila siku.
Utakatifu ambao mteule anauonyesha kanisani inatakiwa utakatifu huo huo auonyeshe nje ya jengo la kanisani.
Maisha ya kuigiza ni Kwa uangamivu Wa muigizaji mwenyewe.
''Wana wetu na wawe kama miche Waliokua ujanani. Binti zetu kama nguzo za pembeni Zilizonakishwa kwa kupamba hekalu. -Zaburi 144:12''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichako chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili

MAISHA YA WOKOVU NDIO KUOKOKA.

BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Wokovu ni nini?
Wokovu ni mpango Wa MUNGU kumuokoa mwanadamu kutoka dhambini, kutoka Katika mambo ya kidunia na kutoka katika hila za shetani.
Kuishi maisha ya wokovu ndio kuokoka kwenyewe.
Isaya 51:6 '' Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na haki yangu haitatanguka.''
Wokovu wa MUNGU ni kwa wateule na Wokovu wa MUNGU ni wa milele.
Watu wengine hudhani wokovu na kuokoka ni mambo mawili tofauti.
Kuna watu pia husema wao wanaishi maisha ya wokovu lakini ukiwauliza kama wameokoka watakuambia hawajaokoka, sijui watu hao wanakwama wapi.
Huwezi kumpokea YESU kisha unaishi maisha matakatifu harafu ukawa bado hujajua tu kama hayo maisha unayoishi ni maisha ya Wokovu na kwa sababu unaishi maisha ya wokovu yaliyo sahihi hakika wewe umeokoka.
Maisha ya wokovu ni maisha ya ushindi dhidi ya dhambi.
Anayeokoa ni mmoja tu ambaye ni BWANA YESU.
Ndio maana Biblia inamwita BWANA YESU jina lake jingine ni WOKOVU WETU.
BWANA YESU anaitwa Wokovu wetu.
Zaburi :27:1 ''BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?''
Faida ya kwanza ya mtu kuishi maisha ya wokovu siku zake zote ni uzima wa milele.
Faida nyingine ni ulinzi wa kipekee wa MUNGU.
Wokovu ni wa milele.
Mtu anayeishi maisha ya wokovu anatakiwa kuishi katika maisha hayo ya wokovu miaka yake yote.
Waefeso 6:17 ''Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la MUNGU;''
Maisha ya wokovu ni maisha matakatifu yanayomtii MUNGU na Neno blake.
Maisha ya wokovu humtii BWANA YESU na injili yake.
Maisha ya wokovu humtii ROHO MTAKATIFU na kila jambo lake.
Matendo 4:12 '' Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.''
Ukitaka kujipima kama unaishi maisha ya wokovu yaliyo sahihi basi angalia matendo yako kama ni matakatifu.
Jambo la pili angalia je unaishi kwa kutii Neno la MUNGU au maneno ya watu.
Jambo la tatu je ROHO MTAKATIFU ana sehemu gani katika maisha yako?
Kumbuka mwanadamu hawezi kuishi maisha sahihi ya wokovu kama mwanadamu huyo hana ROHO MTAKATIFU.
Biblia inahimiza jambo hilo ikisema;
''Tukiishi kwa ROHO, na tuenende kwa ROHO.-Wagalatia 5:25''
Wokovu ni muhimu Sana Kwa watu wote.
Wokovu uko pekee katika BWANA YESU.
Wokovu umekamilika.
Wokovu hujilinda wenyewe.
Wokovu hauhitaji nyongeza maana umekamilika.
Ndugu zangu, ni vizuri sana kila mmoja wetu akaishi maisha matakatifu ya wokovu.

Aliko BWANA YESU ndiko huko wokovu iliko.
Kama huna BWANA YESU Moyoni mwako hakika huna wokovu.
Kama huna Wokovu wa KRISTO hakika huna uzima wa milele.
Aliko BWANA YESU ndiko huko uliko na wokovu wake.
Luka 19:9 ''YESU akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.''
BWANA YESU huambatana na wokovu wake. Tukimpokea BWANA YESU tumeupokea na wokovu wake.
Tukiishi maisha matakatifu ya wokovu hakika BWANA YESU yuko upande wetu.

Kwa Tuliookoka na Tunaoishi maisha matakatifu duniani.
-Makao yetu yako mbinguni, ni makao yasiyoharibika

Mathayo 6:19-21 ''Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako. ''
-Wateule wa KRISTO tutakuwa wa milele.
-Mbingu ni ya milele.
-Vitu vya mbinguni ni vya milele.
-Furaha ya milele
-Na uzima wa milele

1 Petro 5:4 ''Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka.''
Kumpokea YESU leo kwa wewe ambaye hujaokoka ni jambo muhimu zaidi kwako.
Kuishi maisha matakatifu siku zote ni hazina yako ya milele.
-Waliookoka tuna baraka ya milele

1 Petro 1:4 '' tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichako chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili

MAMBO SABA(7) YA KUFANYA WANANDOA ILI WAIFANYE NDOA YAO IWE KIELELEZO.



BWANA YESU atukuzwe mpendwa.
Karibu nikujuze Neno la MUNGU.
Leo nazungumzia ndoa takatifu.
Ndoa ni makubaliano rasmi matakatifu kati ya Mwanaume na Mwanamke kuishi pamoja kama mke na mume, kwa kuanza na utakatifu na kumaliza wakiwa watakatifu.
Ndoa takatifu ni kati ya Mwanaume mtakatifu na Mwanamke mtakatifu watakapoamua kufunga ndoa takatifu katika MUNGU aliye Mtakatifu.
MUNGU anasema;
'' Kwa hiyo mtayashika maagizo yangu, na kuyafanya; mimi ndimi BWANA.-Walawi 22:31''
Ndoa ni agano takatifu la siku zote za kuishi kwa wawili hao.
Ndoa takatifu inatakiwa iambatane na utakatifu.
Ndoa takatifu inaanza na Wokovu wa BWANA YESU na kuishi kwa kulitii Neno la MUNGU.
Yakobo 4:7 ''Basi mtiini MUNGU. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.''
Kuna ndoa zilianzia bar, wanandoa hao wanatakiwa watubu na kuanza kuishi maisha matakatifu ya wokovu wa BWANA YESU.
Kuna ndoa zilianzia vichakani, wanandoa hao wanatakiwa watubu na kuanza kuishi maisha matakatifu ya Wokovu wa BWANA YESU.
Ndoa ili iwe takatifu ni lazima iambatane na utakatifu wa wanandoa husika.
Kuna ndoa ni vielelezo vizuri kwa wengine lakini kuna ndoa ni vielelezo vibaya kwa ambao wanataka kuingia katika ndoa.
Ndoa kuwa kielelezo ni kuwa ndoa ya mfano unaotakiwa kuigwa.
Ndoa ni takatifu sana hivyo inatakiwa iwe baraka na sio balaa.
Waefeso 5:31 '' Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.''
Ili wanandoa waifanye ndoa yao iwe kielelezo Chema kwa wengine inabidi wafanye yafuatayo;
1. Inabidi wanandoa kila mmoja kuiheshimu ndoa.
Waebrania 13:4-5 ''Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi MUNGU atawahukumia adhabu. Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.''
-Anayeiheshimu ndoa yake hataisaliti kwa vyovyote na kwa lolote.
-Anayeiheshimu ndoa yake atavumulia hata kama uchumi hauko sawa kwa wakati huo.
-Anayeiheshimu ndoa yake hatalaghaiwa na pesa ili aisaliti ndoa yake.
-Anayeiheshimu ndoa yake ataiombea ndoa yake maana ahadi ya MUNGU ni kwamba hatawapungukia.

2. Kila mwanandoa kuwa huru ndani ya ndoa.
Wagalatia 5:13 ''Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.''
-Wanandoa wakristo wamewekwa huru mbali na dhambi na tena kwa sababu wako huru basi sio watumwa wa dhambi.
Mwanandoa kuwa huru maana yake ni yule anayeutumia uhuru wake vizuri, kwanza kwa kumhofu MUNGU na pili kwa sababu anautaka uzima wa milele.
Uhuru mwingine kwenye ndoa ni uhuru wa haki katika ndoa.
Lazima mama awe na uhuru kwenye ndoa yake na baba awe na uhuru kwenye ndoa yake.
Wagalatia 5:1 ''Katika ungwana huo KRISTO alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.''
Hakuna haja ya mama hadi amsubiri baba aje atoe kibali ndipo siku hiyo familia wale wali.
Hakuna haja ya baba kuchelewa kidogo tu kazini basi tendo la ndoa linafutwa kwa mwezi mzima.
Kama wanandoa wanaojitambua inabidi kwanza kila mmoja awe na uhuru kwenye ndoa yake. Kushauriana ni muhimu sana lakini isiwe utumwa kwenye ndoa.
Mama asiwe mtumwa na baba asiwe mtumwa katika ndoa bali wote wawe huru wakimpendeza kwanza MUNGU kisha ndoa yao.
Warumi 6:22 '' Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa MUNGU, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele.''

3. Kila mwanandoa kuishi maisha matakatifu.
1 Petro 1:15 ''bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;''
-Maisha matakatifu kwa wanandoa ni mtaji wao wa kuifanya ndoa yao iwe kielelezo kwa watu walio nje.
-Maisha matakatifu kwa wanandoa ni kinga yao ya kuifanya ndoa yao isishambuliwe na adui.
-Maisha matakatifu ni mwanga wa kuwamulikia wanadoa katika njia yao ya maisha yote ya duniani.
Maisha matakatifu ndilo jambo muhimu zaidi kwa kila mwanadamu akiwemo mwanandoa katika maisha yote ya duniani.

4. Kila mwanandoa kumuona mwenzi wake kuwa ni bora kuliko nafsi yake.
Wafilipi 2:3-4 ''Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.''
-Mke akimuona mume wake ni bora kuliko nafsi yake na mume naye akamuona mke wake ni bora kuliko nafsi yake hakika ndoa hiyo itakuwa kielelezo chema mbele ya jamii.
-Kumuona mwenzako ni bora kuliko nafsi yako ni kuifanya ndoa yenu kuwa na afya njema ya kuwafanya muishi kwa amani muda mrefu sana.
-Mume akiwa anamjali zaidi mkewe badala ya kujijali yeye hakika ataleta furaha kwa mke na kuleta furaha kwenye ndoa.
-Mke kama atamjali mumewe na kumuombea daima hakika jambo hilo litaleta baraka kwenye ndoa na amani na furaha kuu.
5. Kila mwanandoa kutii utaratibu mwema waliojiwekea ndani ya ndoa yao.
-Kuna ndoa zimejiwekea utaratibu mzuri katika ndoa yao.
Kuna ndoa zimejiwekea hata utaratibu wa kukutana kimwili, kusaidia wazazi, kutembelea ndugu, kufunga na kuomba.
Ni vizuri pia kama kila mhusika ataufuata utaratibu waliojiwekea wenyewe kwa furaha zao.
Kama ndoa yenu mmejiwekea taratibu mbalimbali ni vizuri sana kujulishana kama mmoja anataka kufanya tofauti au kama kuna dharula.
Kama wanandoa mnaomcha MUNGU mtajiwekea utararibu au mipango ya muda fulani basi ni muhimu sana mkamhusisha na MUNGU katika mipango yenu ili awafanikishe.
Baada ya kuipanga mipango hiyo mnatakiwa kila mmoja wenu aiheshimu ili mtafaruku wowote usitokee.
Kufanya hivyo ni kuifanya ndoa kuwa kielelezo maana majirani hawatasikia hata siku moja mkizozana baada ya mmoja wenu kuvunja utaratibu.
Ni muhimu mkawa na mawasiliano ya mara kwa mara na kujulishana katika yote kwa upendo na amani ya KRISTO.
Wakolosai 3:14-15 ''Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu. Na amani ya KRISTO iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani''
6. Kila mwanandoa kuzingatia usafi wa mwili na roho
2 Kor 7:1 ''Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha MUNGU.''
-Ni muhimu sana kila mwanadoa kuwa msafi wa mwili na roho.
Usafi wa mwili ni usafi wa mwili na kila unachovaa katika mwili.
Usafi wa roho ni kuishi maisha matakatifu.
Ni muhimu sana kuwa watakatifu.
Uchafu kwa mmoja wa wanandoa unaweza kuleta kero kwa mwenzi wake.
Kila mtu anajua usafi ni nini hivyo ni muhimu sana kuwa wasafi wa mwili na roho.
7. Kila mwanandoa kuhakikisha ndani ya ndoa yao KRISTO ni yote katika wote.
Warumi 8:10-14 ''Na KRISTO akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki. Lakini, ikiwa ROHO yake yeye aliyemfufua YESU katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua KRISTO YESU katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa ROHO wake anayekaa ndani yenu. Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili, kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa ROHO, mtaishi. Kwa kuwa wote wanaoongozwa na ROHO wa MUNGU, hao ndio wana wa MUNGU''
-KRISTO ni pekee wa uzima wa milele.
Huwezi ukautaka uzima wa milele harafu humtaki KRISTO.
Mwanandoa makini ni yule anayemtii KRISTO na Neno lake.
Msingi wa ndoa yenu unatakiwa uwe BWANA YESU.
Kuishi kwa ndoa yenu kunatakiwa kuwe kwa utukufu wa MUNGU.
Ndoa yenu inatakiwa iwahubirie wengine uzuri wa WOKOVU.
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichaka chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.

IMANI YA UZIMA IPO MOJA TU, ISHINDANIE.


( Waebrania 12:2, tukimtazama YESU, mwenye
kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu;
ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele
yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu,
naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi
cha MUNGU.)
Leo nazungumzia kuishindania Imani ya uzima
ambayo ipo moja tu.
-Imani Ya Uzima Hushindaniwa.
- Imani Ya Uzima Ipo Moja Tu Yaani Wokovu
Wa YESU KRISTO, Biblia inasema

Matendo 4:12 ''Wala hakuna wokovu katika
mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina
jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu
litupasalo sisi kuokolewa kwalo.''

-Ni jina la YESU KRISTO pekee, hiyo ndio imani
ya pekee ya uzima, na imani hii ya uzima
lazima tuishindanie.
Imani hiyo ya uzima ni moja tu na chanzo
chake ni kulisikia neno la KRISTO na kumpokea
kama BWANA na MWOKOZI wako na baada ya
hapo unatakiwa ujiunge na wana kanisa
wengine katika kuukulia wokovu na kuomba.

''Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na
kusikia huja kwa neno la KRISTO.-Warumi
10:17''

-Hiyo ndio imani ya kweli ambayo unaipokea
baada ya kulisikia Neno la KRISTO YESU na sio
vinginevyo.
Ndugu, shika yote yanayoelekezwa katika Imani
ya KRISTO kupitia Biblia maana yaliyo nje na
KRISTO ni dhambi.

''Na kila tendo lisilotoka katika imani ni
dhambi.Warumi 14:23b''

Imani Haishindaniwi Kwa Mapigano Bali Kwa
Matendo Mema Ya Kumpendeza MUNGU tukiwa
ndani ya imani hii ya uzima.
Hatutakiwi kuitwa tu wakristo bali tunatakiwa
kuitwa wakristo walio na KRISTO ndani yao. Ni
imani ya ndani kabisa ya moyo wa mtu, ni
uhusiano wa ndani kabisa kati ya mwanadamu
na muumba wake.
Ukiipokea imani hii ya uzima , Biblia inasema
hivi

''Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO
amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita
tazama! Yamekuwa mapya.-2 Kor 5:17''

Kwanini Tunatakiwa Tuishindanie Imani Ya
KRISTO?
= Ni Kwa Sababu Ndio Imani Pekee moja tu Ya
Uzima Wa Milele

Yuda 1:3 ''Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii
sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni
wetu sisi sote, naliona imenilazimu
kuwaandikia, ili niwaonye kwamba
mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu
mara moja tu. ''

=Ni kwa sababu kuna wakati mwingine kuna
kupita kwenye nyakati ngumu na kupingwa.

Wafilipi 1:27-29 '' Lakini mwenendo wenu na
uwe kama inavyoipasa Injili ya KRISTO, ili,
nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo,
niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara
katika roho moja, kwa moyo mmoja
mkiishindania imani ya Injili; wala hamwaogopi
adui zenu, katika neno lo lote; kwao hao ni
ishara mathubuti ya kupotea, bali kwenu ninyi
ni ishara ya wokovu, huo utokao kwa MUNGU.
Maana mmepewa kwa ajili ya KRISTO, si
kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake; ''

-Katika Imani Yetu Ya Uzima Tunatakiwa
Kujitahidi Sana Katika Yale Yanayompendeza
MUNGU.

2 Petro 1:5-11 ''Naam, na kwa sababu iyo hiyo
mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani
yenu tieni na wema, na katika wema wenu
maarifa, na katika maarifa yenu kiasi, na katika
kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu
utauwa, na katika utauwa wenu upendano wa
ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.
Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa
tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si
watu wasio na matunda, kwa kumjua BWANA
wetu YESU KRISTO. Maana yeye asiyekuwa na
hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu vilivyo mbali,
amesahau kule kutakaswa dhambi zake za
zamani. Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi
kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu;
maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.
Maana hivi mtaruzukiwa kwa ukarimu kuingia
katika ufalme wa milele wa BWANA wetu,
Mwokozi wetu YESU KRISTO.''.

-Tunaposema Tunaishindania Imani Maana
Yake Tunafanya Yale Tu Yanayokubalika Na
Imani Hiyo Ya Uzima.
-Kwenye Imani Ya Uzima Lazima Tujue
Kwamba Tunashindana Na Maadui Ambao
Wanataka Kututoa Kwenye Imani Hiyo Pekee Ya
Uzima
Maadui Hao Ni
-Shetani Na Majeshi Yake,
-Dunia Na Anasa Zake
-Pamoja Na Mwili Na Matakwa Yake.
Hivyo Tukijua Tuko Kwenye Mashindano Na
Tuvumilie Maana Tumepewa Imani Sio Kuamini
Tu, Bali Na Kuishindania Na Kuteswa Pia Kwa
Ajili Ya Imani

Wafilipi 1:29 ''Maana mmepewa kwa ajili ya
KRISTO, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa
ajili yake;.''

-Katika Imani Lazima Tuzae Matunda Na
Kumpendeza MUNGU.

Wakolosai 1:10 ''mwenende kama ulivyo wajibu
wenu kwa BWANA, mkimpendeza kabisa;
mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi
katika maarifa ya MUNGU; ''.

-Katika Imani Lazima Kusaidiana Kiroho.
Wafilipi 4:3-6 '' Naam, nataka na wewe pia,
mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa
maana waliishindania Injili pamoja nami, na
Klementi naye, na wale wengine waliotenda
kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo
katika kitabu cha uzima. Furahini katika
BWANA sikuzote; tena nasema, Furahini. Upole
wenu na ujulikane na watu wote. BWANA yu
karibu. Msijisumbue kwa neno lo lote; bali
katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja
na kushukuru, haja zenu na zijulikane na
MUNGU. ''

Shika Imani Ya Uzima Daima siku zote wala
usisitesite.

MUNGU anasema.
''Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani;
Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha
naye.- Waebrania 10:38''

MUNGU aliye hai akubariki.
By Peter M Mabula.

KUISIKIA, KUITII NA KUITUNZA SAUTI YA MUNGU.



BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tena karibu sana tujifunze Neno la MUNGU aliye hai.
Kumb 4:35-36 ''Wewe umeonyeshwa haya, ili upate kujua ya kuwa BWANA ndiye MUNGU, hapana mwingine ila yeye. Kutoka mbinguni amekusikizisha sauti yake, ili akufundishe; na juu ya nchi alikuonyesha moto wake mkuu; ukasikia maneno yake toka kati ya moto.''
MUNGU alisema na watu wa Israeli kama ambavyo pia anaweza kusema na wewe leo.
Sauti ya MUNGU waliisikia kama ambavyo leo MUNGU anaweza kusema na wewe kwa sauti yake na wewe ukaisikia.
Licha ya MUNGU kusema na watu lakini sio wote huitii sauti ya MUNGU na sio wote huitunza sauti ya MUNGU.
Sauti ya MUNGU huendana na Neno lake MUNGU yaani Biblia.
Kwa sababu Biblia ni ya MUNGU, MUNGU anaposema na sisi haendi kinyume na Neno lake Biblia.
Siku moja watu waliisikia sauti ya MUNGU ikimthibitisha Mwokozi wa ulimwengu, YESU KRISTO.
Marko 1:11 '' na sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.''
Ni kweli MUNGU husema na watu wake lakini Lakini nataka uelewe mambo haya muhimu kwamba.
Kuna tofauti kati ya kuisikia sauti ya MUNGU, Kuitii sauti ya MUNGU pamoja na kuitunza sauti ya MUNGU.
=Kuna watu huwa wanaisikia sauti ya MUNGU ila hawaitii.
=Kuna watu huisikia sauti ya MUNGU na kuitii kwa muda kisha wanasahau.
=Kuna watu huisikia sauti ya MUNGU kisha wanaitii na kisha wanaitunza.
Hao kundi la mwisho hufanya vyema sana

Luka 9:35 ''Sauti ikatoka katika wingu, ikisema, Huyu ni Mwanangu, mteule wangu, msikieni yeye.''
Sauti ya MUNGU ilisikika kwa wanadamu kwamba MUNGU anataka wanadamu wote wamsikie YESU KRISTO, Wamtii na washike kile anachokiagiza.
Sauti ile ya MUNGU hata leo iko wazi sana kwa kila mtu anayesoma Biblia.
Je wewe licha ya kuisikia sauti ya MUNGU.
Je unaitii sauti ya MUNGU?
Je unaitunza sauti ya MUNGU ili hata ushawishi mbaya ukija kwako sauti ya MUNGU uikumbuke na kukataa ubaya huo?
Waebrania 3:12-15 ''Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na MUNGU aliye hai. Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi. Kwa maana tumekuwa washirika wa KRISTO, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho; hapo inenwapo, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha.''
Ni muhimu sana kuitunza sauti ya MUNGU.
MUNGU husema na wewe kwa njia nyingi sana.
Alivyosema MUNGU jana inaweza kuwa tofauti kabisa na atakavyosema leo.
Kama ulikariri MUNGU aseme na wewe kwa ndoto kama alivyosema na wewe jana, leo MUNGU anaweza kabisa akasema na wewe kwa njia ya Neno lake wala sio ndoto kama ulivyokariri.

Isaya 40:28 ''Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye MUNGU wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.''
Akili za MUNGU hazichunguziki hivyo anaweza kutumia njia nyingi tu ili wewe uisikie sauti yake.
Lengo la MUNGU kusema na wewe ni ili utii kile cha MUNGU na sio kile cha wanadamu.
MUNGU anaposema na wewe jambo fulani na kukuhakikisha kwamba hilo utalipata, haina maana kwamba vikwazo na changamoto havitakuwepo, bali vitakuwepo lakini Kwa sababu MUNGU alisema na wewe, na wewe hujaondoka katika agano hilo la MUNGU basi hakika jambo hilo utalipata.
Changamoto unazokutana nazo ni kuhakikisha tu huitunzi sauti ya MUNGU, Lakini mpendwa nakuomba sana usonge mbele huku ukiitunza sauti ya MUNGU.

MUNGU alisema na Musa juu ya mipango yake MUNGU ya kuwatoa waisraeli Misri.
Musa aliitunza sauti ya MUNGU japokuwa Farao aliita wachawi wote wa Misri wamkwamishe Musa. Lakini Musa aliitunza sauti ya MUNGU na akashinda

Wako watu MUNGU alisema nao.
Kwa miaka kadhaa waliitunza ile sauti ya MUNGU.
Waliitii sauti ya MUNGU na hawakwenda kinyume na Wokovu wa KRISTO.
Baadae waliiacha ile sauti ya MUNGU hata hawakuitunza na mwisho wao ukawa mbaya hata kama mwanzo walisimama katika kweli.

Yakobo 4:7-8 ''Basi mtiini MUNGU. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni MUNGU, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.''
Ndugu, Ni muhimu sana kuitunza sauti ya MUNGU na kuitii siku zote.
MUNGU wakati mwingine hutushirikisha mipango yake.
Mfano anaweza kukuambia kuwa anataka kumuokoa kijana fulani au binti fulani.
Kwa sababu MUNGU amekushirikisha wewe basi unatakiwa wewe ukamhubiri yule kaka au dada uliyemuona ambaye MUNGU anataka kumuokoa.

Sababu za MUNGU kumuokoa ndugu huyo anazijua MUNGU na sio wewe.
Mara nyingi sana MUNGU husema na wewe kupitia Neno lake mfano kama unavyojifunza ujumbe huu.
MUNGU anaposema na wewe kwa Neno lake ni muhimu kumtii MUNGU na Neno lake.
Neno la MUNGU ni la MUNGU tu.
Neno la MUNGU linajua Yote.
KRISTO ni Neno juu ya Neno la MUNGU.
MUNGU anatutakasa kwa Neno.

Ukweli Ni Kwamba Kila Agizo Analotoa MUNGU Ni Agizo Halali Siku Zote.
Jitahidi Sana Kuipenda, Kuishika Na Kuitii Sauti Ya BWANA Na Sio Sauti Za Wanadamu.
Uhakika wetu uko katika Neno la MUNGU hivyo MUNGU anaposema na wewe kwa njia ya Neno haijalishi ni kupitia nani basi tii Neno la MUNGU maana Neno la MUNGU siku zote hutuelekeza kwenye Mema tu aliyotuandalia BWANA YESU.
2 Timotheo 2:15 ''Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na MUNGU, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.''

Japokuwa wakati mwingine adui huleta sauti zake ili kuwapoteza watu wa MUNGU, Lakini kama ROHO MTAKATIFU yumo ndani ya mteule huyo hakika janja ya shetani itajulikana.
Ni Muhimu kujua kwamba Kuna Sauti Takatifu Na Kuna Sauti Isiyo Takatifu Hata Kama Kibinadamu Hiyo Sauti Isiyo Takatifu Kwa Baadhi Ya Watu Itaonekana Takatifu. shetani hujaribu kuiga utakatifu lakini kwa sababu ROHO MTAKATIFU yuko kwetu hakika lazima tutazijua hila za shetani.
2 Kor 2:11 '' Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.''
Shetani naye hutuma mawakala wake ili kuwapotosha watu wa MUNGU lakini tunayo mamlaka kuu ya jina la YESU KRISTO na kwa hiyo mamlaka tunashinda hila za shetani.
Kuna Sauti Ya Kumtoa Nyoka Pangoni Na Kuna Sauti Ya Kumuua Nyoka Huko Huko Pangoni. Sauti Ya Kumtoa Nyoka Pangoni Ni Sauti Ya Watambikaji, Wasihiri, Waganga Na Wachawi Ikiambatana Na Udi Na Ubani Lakini Sauti Inayomuua Nyoka Pangoni Ni Sauti Ya Maombi Katika Jina La YESU KRISTO Ikiambatana Na Damu Ya YESU KRISTO.
Heri Kumuua Nyoka Kuliko Kumtoa Pangoni.
Nyoka Ni Majini, Vibwengo, Mapepo, Mizimu Na roho Za shetani Zote.
Haribu Nyoka Na Sio Kumcheka Nyoka, Omba Na Utashinda Kwa Jina La YESU KRISTO.
Warumi 16:20 '' Naye MUNGU wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya BWANA wetu YESU KRISTO na iwe pamoja nanyi. [Amina.] ''
Sijui Kama Unaijua Hii, Lakini Kama Uijui Ni Kwamba; Kwa Baadhi Ya Mambo MUNGU Akikuambia Jambo Usilitekeleze Hakuambii Jambo Jipya Mpaka Utakapolifanyia Kazi Lile Alilokuambia Mwanzo.
Binafsi Huwa Najitahidi Sana Kufanyia Kazi Kile Anachoniambia BWANA Ili Nipate Nafasi Ya Kuambiwa Kingine.
Mfano Ni Huu, Kuna Watu MUNGU Aliwaambia Watubu Wao Wakopotezea, Lakini Kwa Sana Wanahitaji Mke/mume Mwema Na Kila Siku Wanatamani MUNGU Aseme Nao Juu Ya Hilo Lakini Mbingu Ziko Kimya Hadi Watakapofanyia Kazi Lile MUNGU Aliwaambia Mwanzo.
Sauti ya MUNGU ikiondoka kwa mtu huwa hairudishwi kwa namna yeyote isipokuwa kwa kutubu toba ya kweli.
MUNGU hurudi baada ya toba ya kweli.
Toba ya Kweli pekee ndio ndio inayoweza kuirudisha sauti ya MUNGU katika maisha ya mtu.
Kumb 28:1-7 '' Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, MUNGU wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, MUNGU wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, MUNGU wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo. BWANA atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba. ''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichaka chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.

DHAMBI HUFUTIKAJE?

Kwaya ya kanisa la PentecosteZanzibar wakiimba.


BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Nakukaribisha tule chakula cha kiroho ambacho ni Neno la MUNGU aliye hai.
Dhambi hufutikaje?
Dhambi hufutika baada ya aliyetenda dhambi hiyo kutubu kwa MUNGU kupitia KRISTO YESU.
1 Yohana 1:6-10 ''Tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli; bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake YESU, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.''
Hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye hajawahi kutenda dhambi.
Kwa sababu wanadamu wote wamewahi kutenda dhambi, dhambi zao kama hawajatubu bado ziko hata kama wamezitenda dhambi hizo miaka zaidi ya 60 iliyopita.
Kumpokea YESU kama BWANA na Mwokozi ndiko kunaweza kumtenga mtu na dhambi zake zote za zamani hata jina lake likaandikwa katika kitabu cha uzima. Hakuna msamaha wa dhambi nje na KRISTO ndio maana kitendo tu cha kukataa kumpokea YESU kama mkombozi ambaye damu yake itakusafisha dhambi zote, kitendo hicho tu ni dhambi ambayo inaweza kumpeleka mwanadamu jehanamu.
1 Yohana 5:11-12 '' Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba MUNGU alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. Yeye aliye naye Mwana(YESU), anao huo uzima; asiye naye Mwana wa MUNGU hana huo uzima. ''
Ndugu, hata kama dhambi yako umeisahau lakini napenda kukuambia kwamba kama hujaitubia dhambi hiyo hakika bado iko na kama hutaitubia na kuiacha bado itaendelea kuwepo, na Biblia iko wazi ikisema mwisho wa wenye dhambi(ambao hawajatubu) ni ziwa la moto
Kiu Huondolewa Na Maji Wala Sio Mchuzi Wa Nyama, Na Dhambi Huondolewa Kwa Damu Ya YESU Wala Sio Kwa Kutawadha Miguu Na Mikono.
Kuna Watu Hufanya Baadhi Ya Vitu Wakidhani Kupitia Vitu Hivyo Watasamehewa Kumbe Sio.
Kuna Watu Ni Wagumu Sana Kutubu Kwa MUNGU, Watu Hawa Hufanya Vitu Fulani Vizuri Wakidhani Kupitia Vitu Hivyo Watasamehewa Kumbe Dhambi Yao Bado Inakaa. Hawa Hujaribu Kama Kuondoa Kiu Kwa Kunywa Soda, Matokeo Yake Hata Kama Wamekunywa Soda 10 Bado Kiu Watakuwa Nayo.
Ndugu Zangu, Dawa Ya Kuondoa Dhambi Ni Kutubu Toba Ya Kweli Na Kuachana Na Dhambi Hizo Tena.
Matendo 3:19 '' Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA;''
Jambo la kujua ni kwamba BWANA YESU Atakaa Kwenye Kiti Cha Enzi, Atakifungua Kitabu Cha Uzima, Kisha Yatasomwa Majina Ya Wanadamu Walioshinda Duniani.
Watu walioshinda duniani ni wale waliompokea YESU, Wakatubu na kuanza kuishi maisha matakatifu.
Hata kama kuna wakati katika maisha yao ya wokovu walijikwaa kwa kutenda dhambi, bado walitubu na kuacha uovu huo na kuendelea mbele na wokovu wa BWANA YESU ulio wa thamani sana.
Je,Unawaza Nini Juu Ya Hilo la kusomwa majina katika kitabu cha uzima?
Kuna watu majina yao yatakuwamo na wengine majina yao hayatakuwemo.
Ambayo majina yao yatakuwa katika kitabu cha uzima hao wataurithi uzima wa milele na ambao majina yao hayatakuwemo watapelekwa ziwa la moto.
Ufunuo 20:12-15 '' Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto. ''
Kuna watu hufanya matendo mema bila kutubu wakidhani kupitia matendo yao mema watasamehewa juu kwa juu bila kutubu, huo ni uongo wa shetani.
Ni muhimu sana kujua kwamba sadaka haiwezi kufuta dhambi.
kuwasaidia yatima na wajane hakuwezi kufuta dhambi.
Sio kwamba vitu hivyo ni vibaya Bali ni vizuri sana ila nataka kupitia ujumbe huu niwasaidie watu wengi ambao wakati wa sikukuu, wakati wa mwisho wa mwaka au wakati wowote hutoa misaada yao kwa wagonjwa, wahitaji, Yatima na wajane wakitumia njia hiyo wakidhani ni njia ya kusamehewa dhambi kumbe wala haiko hivyo.
dhambi inafutwa kwa damu ya YESU tu baada ya mwenye dhambi kutubu.
Najua kabisa matajiri wengi hawajaokoka lakini hutumia zawadi kwa wahitaji kama njia yao ya kutaka kutakaswa baada ya uovu mwingi walioutenda. hata hivyo ukweli wa MUNGU ni kwamba sadaka au msaada kwa watu haufuti dhambi Bali ukitaka dhambi zako zifutwe basi nenda kanisani ukaokoke na kutubu.
pia usiache kuwasaidia wajane, Yatima na wahitaji maana ni jambo jema sana ingawa haliwezi kufuta dhambi.

BWANA YESU anasamehe dhambi na atakuandika jina lako kwenye kitabu cha uzima kama ukimpokea na kutubu.
Marko 2:10 '' Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi ''
Inawezekana Malengo Yako Wiki Ijayo Unataka Kwenda Kwa Mganga Sangoma Gwiji, Lakini Taarifa Muhimu Leo Ni Kwamba Hayo Ni Malengo Feki Na Ya Kishetani.
Mathayo 3:2 ''Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. ''
Habari za ufalme wa MUNGU zinahubiriwa.
Wenye masikio ya kusikia wanasikia, wenye kufunguliwa wanafunguliwa.
Lengo kuu la ufalme wa MUNGU ni watu wapate uzima wa milele.
Mfalme wa ufalme wa MUNGU na BWANA YESU na yuko tayari kumuokoa mtu yeyote atakayependa kuokoka.

Hutachuma Matunda Katika Mti Wa Mwenzako Bali Utachuma Matunda Katika Mti Wako. Kama Matunda Ya Mti Wako Yanaitwa Dhambi Ni Hayo Utakayo Kula Baadae, Ni Hayo Yatakuliza Baadae Kama Hutatubu. Kila Mtu Matendo Yake Ndio Hutengeneza Matunda Ambayo Mtu Huyo Atakula Baadae.
Kuna Watu Wana Juhudi Lakini Sio Juhudi Katika MUNGU Aliye Hai. Mtu Anaweza Kuwa Na Juhudi Ya Kuabudu Kila Baada Ya Robo Saa Lakini Kama Hamwabudu JEHOVAH Juhudi Zake Huyo Mtu Ni Bure Na Hazitamsaidia Lolote. Unakuta Mtu Hajawahi Kukosa Kipindi Cha Mafundisho Kanisani Lakini Kama Mtu Huyo Hautaki Wokovu Wa BWANA YESU Juhudi Yake Mtu Huyo Ni Bure. Hakikisha Unakuwa Na Juhudi Katika MUNGU Aliye Hai Sio Kuwa Na Juhudi Katika Vinyago Na Kuabudu Miungu.
1 Kor 10:14-15 ''Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu. Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo. ''

Kuna Watu Wana Wokovu Wa Msimu.
Wakati Wa Matatizo Anaokoka, MUNGU Akimuondolea Matatizo Anarudi Kuwa Mpagani.
Ndugu Nakuonya Katika Jina La YESU KRISTO.
Kama Umeamua Kuwa Wa Shetani Hakikisha Unakuwa Wa Shetani Hata Wakati Wa Matatizo Na Kumbuka Kuwa Kuendelea Kuwa Upande Wa Shetani Huwa Kuna Jehanamu Baadae, Kama Umeamua Kuwa Wa BWANA YESU Hakikisha Unakuwa Mtakatifu Hata Wakati Wa Raha. Mwenye Sikio La Kusikia Na Asikie Leo.
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichaka chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.